BRAND       

 

 

 

IRINGA KWANZA

 

 

BIASHARA YA KARANGA ZA MAYAI

Jinsi ya kupika Karanga za mayai za biashara

Uncategorized
17. Feb 2025
29 views
BIASHARA YA KARANGA ZA MAYAI

BIASHARA YA KARANGA ZA MAYAI

Mahitaji

Karanga 1kg

 

Mayai 2/3 itategemeana na ukubwa wa mayai

 

Sukari vijiko 6 vya chakula

 

Unga wa ngano robo kilo

 

Chumvi kijiko 1 cha chakula

Vanilla au hiliki (inasaidia kuzipa harufu nzuri karanga zako)

 

Mafuta ya kukaanga lita 1

 

Jinsi ya kuandaa

Gonga mayai koroga kwenye kikombe

 

Mimina sukari, chumvi, vanilla kisha endelea kukoroga mpaka mchanganyiko uwe mzuri

 

Weka karanga kwenye chombo 

 

Miminia mchanganyiko wa mayai na sukari kwenye karanga

 

Koroga mpaka zichanganyike vizuri

 

Weka unga wa ngano kidogo kidogo uuku unakoroga.

 

Ukishakuwa mkavu fanya kuupepeta ili ziachane ziwe karanga moja moja

 

Weka mafuta jikoni

 

Moto usiwe mkali sana.

 

Mafuta yakishapata moto kiasi weka karanga.

 

Zingatia kugeuza mara kwa mara ili zisiungue.

 

Zikishabadilika rangi kidogo kuwa kahawia zitoe. 

 

Zichuje mafuta, ziache zipoe. 

 

Hapo tayari kwa kuliwa. 

 

 USHARI KWA MFANYABIASHARA

Usafi wakati wa maandalizi ya upishi wa karanga.

 

Chambua karanga vizuri toa uchafu wote.

 

Usiache karanga zikaungua zitakuwa chungu sana

 

Vipimo: wakati wa kufungasha karanga kuwa makini hakikisha unapima vizuri ili upate faida na wateja wako waridhike pia. 

 

Tafuta soko la biashara yako madukani, mtaani, mashuleni, sokoni. 

 

 

Tafuta wateja popote unapokuwa, tembea na bidhaa zako

 

Comments

No comments has been added on this post

Add new comment

You must be logged in to add new comment. Log in